Quantcast
Channel: News – eNCA Online TV
Viewing all 784 articles
Browse latest View live

TANAPA YATANGAZA KAMPENI YA MIEZI SITA KUHAMASISHA UTALII WA NDANI.

$
0
0

Kaimu Meneja Masoko wa Shirika la Hifadhi za Taifa,TANAPA,Victor Ketansi akizungumza na wanahabari(hawako pichani) juu ya Kampeni ya uhamasishaji wa utalii wa ndani kwa wazawa itakayodumu kwa muda wa miezi sita.
Baadhi ya Maofisa kutoka Shirika la Hifadhi za Taifa,TANAPA, pamoja na Wizara ya Maliasili na Utalii wakizungumza na wanahabari (hawako pichani ) juu ya kampeni ya kuhamasisha wananchi kutembelea hifadhi za taifa ambapo katika kipindi cha miezi sita watakao tembelea zaidi ya Hifadhi nne watapata ofa ya kutembelea Serengeti ikiwa ni pamoja na kugharamiwa maradhi katika hoteli yenye hadhi ya nyota tano.
Kaimu Meneja Mauzo wa TANAPA,Victor Ketansi akisisitiza jambo.

Mkuu wa Idara ya Utali katika Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro,Eva Mallya akizungumza vivutio mbalimbali vunavyopatikana katika hifadhi ya taifa ya Mlima Kilimanjaro.

Mwakilishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii ambaye pia ni afisa utalii mfawidhi na mkuu wa kanda ya utalii Kaskazini,Lauriano Munishi akizungumza jambo mbele ya wanahabari(hawako pichani)juu ya uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha utali wa ndani.
Mkuu wa Idara ya Utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Arusha,(ANAPA) Neema Philip akizungumzia vivutio mbalimbali vinayopatikana katika hifadhi ya Arusha.
Afisa Utalii Mwandamizi katika Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi ,Pellagy Marandu akizungumzia vivutio mbalimbali vinavyoopatikana katika hifadhi hiyo.
Meneja Mawasiliano Mwandamizi wa Shirika la Hifadhi za Taifa,TANAPA,Catherine Mbena akiwa na mwandishi wa habari wa TBC Kilimanjaro,Sauda Shimbo wakati wa kikao cha maofisa wa TANAPA na wanahabari kuzungumzia juu ya kampeni ya kuhamasisha wananchi kutembelea hifadhi za taifa .

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini..


NEWS: Joh Makini (@JohMakini) (Tanzania) Collaborates with AKA (@akaworldwide) (South Africa)

$
0
0

IMG-20150824-WA0010

Johmakini collaborates with AKA from South Africa under the production of ‘Nahreel’ of The Industry Studios. During AKA’s visit to Tanzania in May, his radio interview on a national radio “Clouds fm” brought up a conversation about him collaborating the multiple Tanzania hip hop award winner Johmakini and The hit maker of NUSU NUSU. The two hit the studio and made it happen same day and made a song called Don’t Bother – Joh Makini ft AKA

The two were recently seen posting pictures in South Africa while shooting the new video.
We cant wait for this collaboration by the two MEGA hiphop artists.

Joh Makini is multiple hip hop award winner of the Kilimanjaro Tanzania Music awards and recently was awarded as best hip hop artist of the year and best hip hop lyricist of the year 2014-2015.

Joh Makini  was the first hip hop artist from Tanzania to hit number one on the MTV base african official chart. Joh Makini attended coke studio season two with Chidinma


Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE

NGOMA AFRICA BAND KUTUMBUIZA VECHELDE FESTIVAL-UJERUMANI JUMAMOSI 5 SEPT 2015

$
0
0

Ngoma Africa band (1)

Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya Ngoma Africa band aka FFU-ughaibuni ukipenda waiite viumbe wa ajabu Anunnaki Alien’s yenye makao kule Ujerumani inatarajiwa kutingisha jukwaa katika maonyesho ya Vechelde Festival nchini Ujerumani Jumamosi 5. September 2015 saa 2:00 Usiku katika eneo la :Bürgerzentrum Vechelde liliopo mtaa Hildesheimer Straße 5 mjini Vechelde jirani mji wa Braunschweig,Ujerumani.Bendi hiyo maarufu Ngoma Africa yenye sifa za kuwatia kiwewe washabiki wa muzikikatika maonyesho ya kimataifa kwa kutumia mdundo wao “Bongo Dansi” made in Uswahilini ndio bendi pekee ya kiafrika barani ulaya iliyoweza kudumu kwa miaka 22 na kufanikiwa kukama soko la kutumbuiza katika maonyesho ya kimataifa. Kwa sasa bendi hiyo inatamba na CD yake mpya ya “LA MGAMBO” yenye nyimbo mbili za kumuaga rais Jakaya Kikwete na CD hiyo utunzi wake Kiongozi wa bendi Ebrahim makunja aka Kamanda Ras Makunja imeshatua nchini Tanzania tayari kwa kutingisha anga katika vituo vya redio mbali mbali.
wasikilize ffu-ughaibuni at www.reverbnation.com/ngomaafricaband

Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE

IMETOSHA Music and Laughters Night

$
0
0

sticker_4.5x4.5

Ndugu zangu,

Nawasalimu katika jina la bwana,

Assalam Aleykum!

Nikianza na neno la shukrani, naomba nizitoe za dhati kwa kunivumilia, na kufanya nami kampeni ya Imetosha katika mazingira magumu sana katika awamu ya kwanza. Hii ni kutokana na ugeni katika uendeshwaji wa taasisi pamoja na uhalisia wa safari za kiharakati, mara nyingi wanaofika safari huwa ni wachache, lakini nyie hamkuwahi kukata tamaa katika kuniunga mkono.

Awamu ya kwanza ya kutambulisha taasisi na misimamo yake imefanikiwa, na sasa tunaenda katika awamu ya pili, ambapo baada ya kufanya matembezi, na kampeni mbali mbali ndogondogo, tulifanikiwa kwa kuungwa mkono na taasisi rafiki na azma ya kwanza ilikuwa ni kukiunga mkono kituo cha Buhangija kilichopo Shinyanga.

Lakini baada ya mimi binafsi kama muasisi na mwenye wazo, kufikiri kwa kina kuhusiana na Shinyanga, ambako kiukweli mazingira yake hayajathibitika kuwa salama, na pili kuwa ni kituo cha serikali, nilikuja na wazo la Taasisi kuwa na kijiji cha mfano ambacho, pamoja na kuhifadhi watu wenye ualbino na wasio na ualbino bali pia kiwe kituo cha uzalishaji mali, ambacho kitawakomboa watu wenye ualbino katika ile dhana na kuomba omba, na kuwa wachangiaji rasmi wa pato la taifa kwa kufanya biashara ya kilimo na ufugaji.

Hivi ninavyoongea tayari tumeshatoa malipo ya awali kwa Mzee idd Shemdoe wa huko Bumbuli, Lushoto, mkoani Tanga ambaye amekubali kuiuzia taasisi shamba la Mikahawa lenye ukubwa wa ekari 50. Hapo taasisi ina mpango wa kufungua kituo kitakachoitwa Santa Lucia, Safe House and Estate.

Eneo litatumika kwa kilimo, ufugaji, pamoja na elimu, kwa maana ya shule kubwa inayofundisha kwa mtaala wa kimataifa, lengo likiwa ni kuwawekea watu wenye ualbino vitega uchumi ambacho vitasababisha wao na taasisi yao kutowapigia wafadhili magoti mara kwa mara na badala yake kuwa sehemu ya watatuzi wa matatizo ya kijamii yanayoiklumba nchi.

Kaka na dada zangu, kuwa na eneo tu haitoshi, na safari ya kuifikia ndoto hii ni ndefu inayochukua muda mrefu kuikamilisha. Mimi naiamini kwa sababu tu nina nia na nimedhamiria kuifanya kama sehemu ya ndoto zangu za kimaisha.

Nachukua nafasi hii kuwaomba kunisaidia kushiriki katika shughuli mbali mbali nitakazokuwa nazifanya katika kutunisha mfuko wa taasisi, na hapa naileta kwenu shughuli ya Music and laughetrs, ambayo Orijino Komedi wamekubali kuwa wenyeji huku muziki nao ukichukua sehemu kubwa ya shughuli.

Hii itakuwa Septemba 11, naomba muwahimize wadau kadri muwezavyo wajitokeze kwa wingi kutuunga mkono kwa umoja wetu.

Mungu ibariki tanzania Mungu aubariki umoja wetu


Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE

Lil Ommy (@LilOmmy) wa Times FM aachia tena Jarida la The Playlist.

$
0
0

Cover Opening Front-and-Back cover Lil Ommy MAMAawards Playlist 03 Playlist Bella Playlist Mganga

MTANGAZAJI wa kipindi cha The Playlist cha 100.5 Times Fm, Lil Ommy (Omary Tambwe) ameendeleza utaratibu wa kutoa jarida maalum la ‘The Playlist’ ambalo linapatikana BURE likiwa na habari za burudani, mahojiano na list ya nyimbo 5 walizochagua Celebrities waliosikika kwenye kipindi hicho. Jarida litatoa nafasi kwa baadhi ya wasikilizaji waliopitwa kuweza kusoma yaliyojiri kwenye show hiyo ya kijanja.

Linapatikana katika Malls mbalimbali, Supermarkets, Salon na Maduka ya nguo bongo, kufahamu zaidi jinsi ya kulipata bure, sikiliza 100.5 Times Fm au follow @LilOmmy kwenye Instagram.

Kwneye jarida hili wamo wakali wa Muziki na Mitindo, Christian Bella, Peter Msechu, Kassim Mganga, Meninah, Tunda76 Video Queen na Top Model Maggie Vampire, wamefunguka mengi ambayo fans wao wangependa kuyafahamu kuhusu maisha yao.

Pia kuna special coverage ya burudani ikiwemo tuzo za Mtv MAMAs, BET Awards 2015, Mashahiri ya wimbo wa Wizkid Ojuelegba, Top 10 Songs, Saa kali na hoverboard ambazo ni kicki ya mjini kwa sasa.

kwa mujibu wa Lil Ommy, THE PLAYLIST Magazine litakuwa likitoka kila baada ya miezi likiwa na Mastori ya wasanii wote walikuja kwenye kipindi chake kwa muda huo. Kwa Mikoani litapatikana pia ila ni Tabora, Mwanza, Dodoma, Tanga, Mbeya na Morogoro kwa sasa.

Usikose kusikiliza The Playlist kila Jumapili saa kumi hadi kumi na mbili jioni ambapo Star anadondoka ndani ya Studio kuchagua ngoma tano kali anazopenda na kupiga interview ya kibabe. #thePLAYlistMagazine


Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE

Mkali wa RnB ASH HAMMAN kuachia video yake ya WAHALA Ijumaa hii tarehe 11

$
0
0

wahala poster square

Mkali wa RnB, Ash Hamman anatarajia kuachia video ya wimbo wake Wahala ijumaa hii ya tarehe 11 mwezi huu.

Video ya Wahala inafuatia kufanya vizuri kwa wimbo huo katika nchi tofauti za Mashariki ya Kati na Afrika.

Ash Hamman, ambaye makazi yake ni Dubai, anajulikana kwa nyimbi zake kali kama ‘Body n Soul’, ‘Im Sorry’ , ‘Over’ na huu wa sasa ‘Wahala’.

Video ya Wahala ambayo inatajwa kama moja ya video ghali zaidi kutengenezwa inatarajiwa kuwavutia mashabiki wengi wa muziki duniani.

Akizungumzia video hiyo ambayo imefanyika Dubai, Ash Hamman alisema wanamuziki wengi wanafanya vitu vinavyofanana hali inayowanyima mashabiki ladha tofauti.

‘Video hii ya Wahala itawapa mashabiki ladha tofauti pamoja na kuikuza sanaa ya utengenezaji wa video katika ubora na maudhui mazuri’ alisema Ash.

Baadhi ya vipande vya nyuma ya kamera za video ya Wahala zimeanza kurushwa na vituo mbalimbali vya televisehni duniani kama MTV na Clouds TV Kimataifa.


 

Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE

Huyu ndiye DJ PIERRA mshindi wa tuzo ya NAFCA 2015 akiwa kama BEST ACTRESS

$
0
0

12004136_652449494892516_7137574295401733326_n

DJ maarufu kutoka Kenya amekuwa akisherekea baada ya kunyakua tuzo ya Nollywood katika filamu aliyoigiza ijulikanayo kama When Love Comes Around. DJ huyo wa kike aliwashangaza wengi kwa kushinda tuzo hiyo, kwa kuwa anafahamika zaidi kwa muziki kuliko uigizaji wa filamu. Hata hivyo alipata tuzo ya muigizaji bora wa kike katika tuzo za Nollywood & African Film Critics Awards jijini Los Angeles, Marekani. DJ Pierra Makena aliigiza kama Didi, mwanamke asiye na bahati na anayetafuta penzi.

e689b7be43da8349d587127328003c4a_XL


Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE

RADIO YA E-FM YAANZISHA SHINDANO LA KANGA KWA WANAWAKE KUPITIA KIPINDI CHA UHONDO

$
0
0

1

Ofisa Habari, Lydia Moyo (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo wakati akimkaribisha Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Redio EFM, Denis Ssebo  kuzungumza na wanahabari. 2

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Redio EFM, Denis Ssebo (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu shindano lililoanzishwa na redio hiyo la Kanga kupitia kipindi cha Uhondo kwa ajili ya wanawake wote wasikilizaji wa redio hiyo ambalo limeanza rasmi jana. Kulia ni Mtangazaji wa kipindi hicho, Dina Marios na Ofisa Habari, Lydia Moyo.

3

Mtangazaji wa kipindi cha Uhondo, Dina Marios (kulia), akizungumzia shindano hilo.

HABARI NA PICHA KWA NIABA YA http://mrokim.blogspot.com


Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE


NEWS: Ushawahi kujiuliza wapendanao hawa VANESSA MDEE na JUX watafanya wimbo wapamoja lini? Jibu liko hapa

$
0
0

Untitled

MKALI wa muziki wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee ‘V Money’ na Juma Jux ‘Jux’, wamesema baada ya kila mmoja kukamilisha kazi zake ndipo watatoa nyimbo zao za ushirikiano ambazo wamesharekodi. Aliongeza kwamba, kutokana na kila mmoja kuwa na kazi zake nyingi, hawataweza kufanya kazi ya pamoja hadi kila mmoja atakapomaliza, maana wazo hilo walikuwa nalo muda mrefu na wameshalifanyia kazi, ingawa hawataki kuzitoa kwa sasa. “Tumeshafanya nyimbo za pamoja nyingi, lakini hatutatoa kwa sasa kutokana na kuwa na kolabo na wasanii wengi, naye kuwa na kazi zake hivyo kila mtu akimaliza ‘project’ zake ndipo tutatoa nyimbo zetu za ushirikiano,’’ alisema V Money.



 

Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE

HUAWEI Y360, KIKI INAYOPEWA INAFANANA NA UBORA WA SIMU HUSIKA?

$
0
0

Katika siku kadhaa zilizopita kumekuwa na matangazo kadhaa hasa kwenye mitandao ya kijamii juu ya simu mpya inayouzwa kwa ushirikiano wa makampuni mawili nguli ya mawasilino nchini. Huawei ambao ni watengenezaji wa simu kwa ushirikiano na Tigo.

Untitled

Baadhi ya watu maarufu wamekua wakiizungumzia kwenye kurasa zao binafsi. Kama unavyooa Dina Maris hapo juu. Kama mtandao wa masuala ya teknolojia, nikaona si mbaya kama tutaitazama simu husika, ili kujua kama YALIYOMO YAMO.

Simu hii inauzwa shilingi 160,000 kwenye maduka ya Tigo ambapo utarudishiwa pesa uliyonunulia kama vifurushi kwa miezi sita. Hii ni ofa nzuri kwa simu yenye sifa hizi.

Simu hii inatumia Android OS, v4.4.4 (KitKat), kioo cha inchi nne na CPU Quad-core 1.2 GHz Cortex-A7. Ina Camera mbili, ya mbele (maalumu kwa SELFIE) ina 2MP na ya nyuma ina 5 MP, 2592 х 1944 pixels, flash mbili.

2

Waswahili husema kizuri hakikosi kasoro, Je kuna kasoro gani nilizoona kwenye simu hii? Ukweli ni kwamba sikuona tatizo lolote. Bei yake ni ndogo sana ukifananisha na sifa za simu hii. Kama unahitaji simu bora kwa gharama nafuu basi hii ni simu kwa ajili yako.


Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE

Tigo na Huawei waungana.

$
0
0

Katika kile kinachoonyesha ni kujipanga vyema, kampuni nguli za mawasiliano nchini Huawei na Tigo wameungana kukukufikishia huduma kwa gharama nafuu na haraka zaidi.

Tigo na Huawei wameungana kukuletea simu za mkononi aina ya Huawei Y360 ambazo zitakua zikiuzwa katika maduka ya Tigo nchi nzima.

1

Katika kujua watanzania wamelipokeaje hili, nilitembelea maduka kadhaa ya Tigo jijini Dar es Salaam kuzungmza na wateja wao.

Aboubakar Msami mkazi wa Temeke anasema

‘Ni simu nzuri ya kipekee, bei yake ni nafuu na zaidi unarudishiwa pesa hiyo kama vifurushi kwa miezi sita. Nadhani ushirikiano huu wa makampuni uwepo mara kwa mara ili kutunufaisha zaidi’

Nae Antony Shirima anayejishughulisha na uuzaji na utangenezaji wa simu Kariakoo jijini Dar es Salaam alikua na haya ya kusema.

‘Niliposikia wanauza hii simu 160,000 nilihisi ni kama utani fulani, huwezi kupata smartphone yenye Android 4.4.2, kamera megapixel 5, ya mbele 2 na kioo cha inchi nne kwa bei hiyo labda ziwe zile za watu wenye macho madogo’

2

Nilimuuliza pia kuhusu ubora wake kwa mtuamiji . Alikua na haya ya kusema

‘Hii simu ni nzuri, CPU yake ni Quad-core 1.2 GHz Cortex-A7 ambayo inaifanya kuwa na kasi sana, pia internal memory yake ya 4GB inakufanya uweze kuitumia bila hata kuweka memory card ya ziada.’

Na je vipi kuhusu kuuzwa kwenye maduka ya Tigo? Hili alilionaje?

‘Nadhani ni jambo jema, kwanza kwa sababu Tigo wana maduka nchi nzima hivyo ni rahisi kwa kila mtu kuweza kuipata bila shida, jambo la pili ni kuwa inakuwa ikitoa uhakika zaidi kwa mnunuzi, siku hizi kuna simu feki nyingi sasa ukinunua kwenye maduka ya Tigo unakua na uhakika umenunua bidhaa salama kwani unapata na warranty’


Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE

NEWS: MSIMU WA BURUDANI WA MTIKISIKO WAZINDULIWA RASMI MKOANI IRINGA.

$
0
0

_DSC0095 _DSC0097 _DSC0112 _DSC0116 _DSC0128 _DSC0155 _DSC0188

Na mwandishi wetu, Iringa.

MSIMU waburudani wa ‘mtikisiko’ unaoratibiwa na kituo cha redio cha ebony kilichopo mjini Iringa, umezinduliwa rasmi tayari kwa kuanza kutoa burudani kwa wakazi wa mikoa minne ya kusini mwa Tanzania ambapo kwa mwaka huu inadhaminiwa na kampuni ya mtandao wa simu za mikononi waTigo

Mtikisiko ambao umekuwa ukipata umaarufu tangu kuanzishwa kwake mwaka 2007 kwa kauli mbiu zake ikiwamo ya mwaka huu isemayo “mtikisiko 2015 tumefika na Tigo ,dhima kubwa ya msimu huo umekuwa ukitumika kurudisha shukrani kwa wasikilizaji, na wateja wa kituo hicho cha redio.

Akizungumza katika uzinduzi wa msimu wa mtikisiko uliofanyika katika kituo hicho cha redio na kurushwa moja kwa moja hewani,mwenyekiti wa kamati ya maandalizi BonnieNyatogo maarufu kwa jina la Bonnie Sly alisema kwa mwaka huu wanatarajia kufanya mtikisiko wa burudani katika mikoa ya Ruvuma Mkoani Njombe katika halmashauri ya mji wa Makambako, Mkoani Mbeya katika wilaya ya Mbeya Mjini, na mtikisiko wa mwisho utafanyika mkoani Iringa.

Bonnie sly alisema kwa mwaka huu wamedhamiria kutoa burudani iliyosheni ubunifu kutokana na maboresho makubwa waliyoyafanya kwenye vifaa, na ongezeko la mkoa wa Ruvuma.

“maboresho tuliyoyafanya mwaka huu ni pamoja na vifaa vya sauti vya kisasa, jukwaa la kisasa, wasanii wachanga na wazoefu,na mambo mbalimbali yanayohusu jamii” alisema Bonnie Sly.

Mratibu wa msimu huo waburudani Edwin Bashir maarufu kwa jina la “Eddo”aliwashukuru wananchi ambao wamekuwa wakijitokeza kwenye viwanja vinavyotoa burudani pamoja na wafanyabiashara na makampuni ambayo yamekuwa yakitoa ushirikino kwa kituo hicho cha redio cha ebony.

….Mwisho.


 

Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE

Tuzungumzie Bundesliga

$
0
0

Hata kama si mpenzi wa soka, ni lazima utakuwa umewahi kusikia majina ya vilabu vikubwa barani Ulaya kama vile Bayern Munich na Wolfsburg Germany. Hivi ni vilabu vikubwa vinavyoshiriki ligi kuu ya Ujerumani maarufu kama Bundesliga

1

Habari hii si kuhusu vilabu wala uchambuzi wa kisoka, lakini ni kuhusu jinsi unavyoweza kuitazama.

Katika pitapita zangu nimekutana na hii application, inaitwa Tenbre inatolewa na Startimes BURE. Unaweza kujiuliza, kuna uhusiano gani kati ya hii Tenbre na Bundesliga?

2

Ukiwa na application hii ya Tenbre unaweza kutazama Bundesliga kwenye simu yako mahali popote wakati wowote. Huu ndio uhusiano uliopo.

3

Kama mdau wa michezo niliona sio mbaya kama nitakufikishia nawe njia rahisi ya kuweza kutazama Bundesliga mahali popote ulipo. Unaweza kuDOWNLOAD application hii hapa http://bit.ly/1iZxj3W bila gharama zozote. Tazama bundesliga BURE.


Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE

PICHA: Wasanii KASSIM MGANGA na JAFFARAI watembelea vituo vya radio DODOMA.

$
0
0

_MG_0468

Leo majira ya jioni wasanii wawili wanaoiwakilisha Bongo Fleva namzungumzia Kassim Mganga pamoja na Jafarai walitia timu katika vituo viwili vya radio kwa hapa Dodoma. Vituo hivyo ni NYEMO FM pamoja na DODOMA FM nia na madhumuni ni kutangaza nyimbo zao mpya pamoja na kufanya show yao ya pamoja usiku huu ndani ya NEW MAISHA CLUB iliyopo hapa Dodoma. Baada ya show hiyo nitawaletea picha na matukio yote yaliyojiri katika show hii yao.

1

Kassim Mganga

2 3

Mkongwe Jafarai

4

DJ Massu kutoka A FM

5

Mtangazaji wa Radio kutoka Dodoma FM

6

Charz meneja wa Kassim Mganga

7

Mtangazaji kutoka Nyemo FM

8 9 10 11 12 13


Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE

JINSI YA KUONGEZA SPEED KWENYE SIMU YAKO.

$
0
0

Moja kati ya matatizo ya smartphones nyingi ni kuwa speed au kasi yake huwa ndogo sana. Hii hutokea mara nyingi kama umefungua applications/programs nyingi kwa mara moja. Je unawezaje kujikwamua na hali hii?

20150918_143620

Kuna njia mbali mbali ambazo unaweza kutumia kuondokana na tatizo la simu kufanya kazi polepole. Njia kubwa na ya uhakika ni KUNUNUA SIMU YENYE UWEZO MKUBWA.

Kununua simu yenye uwezo wa kufungua application nyingi kwa wakati mmoja bila kusumbua ndio dawa sahihi ya kuondoka na tatizo hilo. Bahati mbaya sana, nyingi kati ya simu zenye uwezo huu huuzwa gharama kubwa na hivyo watu wengi wa kawaida hushindwa kuzipata.

Hata hivyo kuna aina mojawapo ya simu ambayo ina uwezo mkubwa na gharama zake ni za kawaida. Hivi karibuni, kampuni ya uuzaji wa simu za mkononi kwa kushirikiana na Tigo wamezindua Huawei y360 ambazo zinauzwa kwenye maduka ya Tigo nchi nzima kwa shilingi 160,000. Pindi mteja anunuapo simu hizo, atarudishiwa pesa yote aliyonunua kama vifurushi mbalimbali kwa muda wa miezi sita.

dd

Huawei Y360 ni simu yenye uwezo mkubwa. Ikipewa nguvu na CPU yenyeQuad-core 1.2 GHz Cortex-A7 uwezo wake wa kufungua applications nyingi kwa mara moja bila kupata shida yoyote. Pamoja na uwez mkubwa wa kufanya kazi, Simu hizi pia zina kamera nzuri yenye 5 MP, 2592 х 1944 pixels, na dual-LED flash (flash mbili).



Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE


NEWS: KHULI CHANA x PATORANKING RELEASE “NO LIE” IN EAST AFRICA

$
0
0

Khuli Chana x Patoranking - No Lie Artwork

Multiple award-winning South African rapper Khuli Chana and Nigeria’s reggae-dancehall artist (Winner 2015 MTV Africa Music Award for Best New Act) – Patoranking officially release the single – NO LIE – in East Africa.

The song produced by EKelly is an effortless yet explosive fusion of the best of hip-hop and dancehall created by two of the best artists in Africa. Touted as one of the hottest collaborations to come out of Africa this year, NO LIE has already hit the number 1 spot in the UK on DJ Edu’s Destination African show #DNATop5 on BBC 1Xtra, and South Africa’s Y FM, among other stations across countries.

Patoranking is glad to release the song in East Africa, ahead of his planned visit to the region and collaboration with East African artists, a venture he only refers to, “a surprise gift to my fans”.

In a breakout streak, Patoranking has enjoyed a string of successful singles including My Woman, My Everything featuring Wande Coal, Daniella Whine and Girlie O Remix featuring Tiwa Savage. His travel and tour has seen him perform in several countries recently. They include Tanzania, Mauritius, America and UK. His debut album is set for release December, 2015.

 Purchase NO LIE via iTunes: https://itun.es/za/Avyx9


 

Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE

Mambo mapya 2015, Watanzania Wanasemaje?

$
0
0

Wiki iliyopita niliweka hapa habari kuhusu simu mpya za Huawei aina ya Huawei Y360. Kama ulikosa habari ile, kwa kifupi ni kuwa makampuni makubwa ya simu za mkononi za Huawei na TIGO wameungana na kuleta simu nchini ambazo zinauzwa kwa bei nafuu ya shilingi 160,000 pekee kwenye maduka ya Tigo nchi nzima huku ukirusishiwa pesa uliynunulia kama vifurushi.

cc

Wiki hii nisingependa kuzungumzia simu tena, ila ni maoni ya Watanzania wa kawaida watumiaje na wasio watumiaji wa simu kuhusu habari ile. Nimekukusanyia maoni hayo hapa chini.

“Baada ya kusoma habari yako, nimenunua simu hii kwenye duka la Tigo Temeke, ni kweli kama ulivyosema, wamenirudishia pesa kama vifurushi ”

Nassoro, Temeke

“Simu ni nzuri sana, hasa kamera yake ndio nimependa na bei yake sio kubwa, wamejitahidi”

Tekla, Dodoma

“Watu wamezichangamkia sana inaonekana, maana siku ya kwanza nimeenda nimekuta foleni watu wananunua. Ni simu nzuri na picha zake nzuri ”

Mariam, Mbeya

96


Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE

Msimamo wa LIGI kuu ya Ujerumani – Bundesliga

$
0
0

Ratiba ya michuano ya soka nchini Ujerumani maarufu kama Bundesliga bado inaendelea. Leo saa 9:30 kutakuwa na mnyukano mkali kati ya Darmstadt 98inayoshikilia nafasi ya tisana Mainz 05inayoshikilia nafasi ya kumi na mbili. Bayern Munich bado wanaongoza msimamo wa ligi wakiwa na point 21.

1

Kwa hapa nchini unaweza kufuatilia michano hii ukiwa na king’amuzi cha Startimes pekee. Lakini kama wewe si mteja wao usitie shaka, kuna njia mbadala unayoweza kutumia kutazama LIVE michuano hii kupitia simu yako ya mkononi tena BURE kabisa.

Unachotakiwa kufanya ni fuata hatua zifuato.

  1. Hakikisha unatumia simu yenye Android, au kama una simu hizi Samsung, Huawei, HTC, Techno, Sony au nyingine yoyote inayotumia Android.
  2. Nenda kwenye Playstore ( unakodownload apps zingine) kisha search neno Tenbre.
  3. Install application ya tenbre, jiunge Bure na Tazama Bundesliga bure.

Usisahau kunipa hapa mrejesho, je umeionaje?

2



Twitter: @chokadj @djchokatv

Instagram: @djchokatv @chokadj @djchokamusic

Facebook Fans Page: https://www.facebook.com/djchokamusic

Download DJChokaMusic Android Application Click HERE

Diamond, Bono na D’ Banj wafanya remix ya wimbo wa Strong Girl

$
0
0

RED_ONE RWANDA_NIGERIA-2241

Diamond Platnumz, mwimbaji kiongozi wa kundi la U2, Bono, D’Banj na Banky W wamefanya remix ya wimbo wa Strong Girl, ambao mwanzo ulifanywa na wanamuziki Vanessa Mdee, Arielle T, Blessing, Gabriela, Judith Sephuma, Selmor Mtukudzi, Victoria Kimani, Waje na Yemi Alade.

Katika remix hiyo iliyozinduliwa wiki hii, muigizaji Omotola wa Nigeria ndiye video queen kwenye video kali ya wimbo huo.

Wimbo huo una lengo la kuwaambia viongozi kutilia mkazo uwezejaji na haki za wanawake katika mkutano wa umoja wa mataifa unaoendelea hivi sasa nchini Marekani.

Katika vikao vya wakuu wa nchi kupitisha maelengo dunia ambayo yataweka ajenda za maendeleo kwa kizazi, mastaa hawa wa muziki Afrika wametoa wito kwa serikali zote zilizokutana mwishoni mwa juma lililopita katika mkutano wa umoja wa mataifa kumweka mwanamke na msichana katika utashi wa maendeleo ya kitaifa na dunia mwaka 2015.

Mwaka huu malengo ya milenia yanafika ukingoni, na kuanzia septemba 25 malengo ya dunia kwa maendeleo endelevu ambayo yanalenga kuweka ajenda ya maendeleo kwa kizazi hiki ambapo tunaweza kushudia kizazi kikubwa chenye kuondoa umasikini uliokithiri. kama alivyowahi kusema Nelson Mandela.

Tayari kuna viashiria vya maendeleo, kwani mapema mwakwa huu Umoja wa Afrika AU wakuu wa nchi waliafiki kushughulika na ukweli kuwa umasikini unaathiri zaidi wanawake.

‘Nawaomba watanzania na waafrika kiujumla wasikilize wimbo huu kwani ukimyanyua msichana na mwanamke, utakuwa umenyanyua kila mtu, na nina hakika viongozi wamesikia wito wetu wa kunyanyua wasichana na wanawake kama ajenda muhimu. Ni wakati wa kutekeleza sasa’ anasema Diamond.

Kurudia wimbo wa Msichana Imara kwa kuwashirikisha wasanii wa kike na kiume si tu unaongeza nguvu ya ujumbe bali unaweka msisitizo wa kumwezesha mwanamke na kuonyesha ushirikiano baina ya wanamme na wanawake kuhakikisha wasichana na wanawake wanainuliwa.

Naye msanii D’Banj, anasema amepata heshima kubwa kuwa mshirika kwenye wimbo huu kwani ni muhimu kwangu kutumia muziki wangu kusaidia mabadiiko ya dunia na kuonyesha kuwa uwezeshaji wa wanawake ni suala la dunia nzima na ndio msingi wa kuondoa umaskini uliokithiri.

‘Wimbo huu ni zaidi ya wimbo au mwimbaji, na ni furaha kufahamu kuwa wakati wanamme ni sehemu ya tatizo, wamekuwa sehemu ya suluhisho’ anasema Bono, mwimbaji kiongozi wa U2.

Tanzania ni nchi muhimu kwa matokeo haya kwa kuwa na ushawishi mkubwa barani Afrika na baadhi ya mifano ya maendeleo kama Mpango mkakakati wa kitaifa kuhusu Maendeleo ya Jinsia (2005). Baadhi ya maeneo yanayohitaji kufanyiwa kazi:

  • Usawa wa kijinsia umeendelea kuwepo kwa mujibu wa UNDP Maendeleo ya usawa wa kijinsia 2013 Tanzania inashikiria nafasi ya 159 kati ya nchi 187.
  • Kuendelea kuwepo kwa maambukizi ya HIV/AIDS, ambayo kwa mujibu wa tume ya Taifa ya UKIMWI, maambukizi kwa wanawake ni (6.2%) kuliko wanamme (3.8%)
  • Haki za Ardhi ni tatizo kubwa kwa wanawake wa Tanzania, wengi wanaathirika na masula hayo na kuathrili haki zao

Processed with VSCOcam with x5 preset

You tubehttps://www.youtube.com/watch?v=v-TGznFHHv0

DIRA YA DUNIA JUMATATU 05.10.2015

Viewing all 784 articles
Browse latest View live